Habari
zilizotufikia kutoka mjini Mtwara Zinasema kuwa Gari lililobeba Shehena
ya Mabomba ya Kusafirishia gesi kutoka Mjini Mtwara kuelekea Dar
limeshambuliwa na mawe na kupelekea dereva Wa lori hilo Kujeruhiwa
Vibaya. Lori hilo lilianza kushambuliwa mara baada ya kuingia katika
manispaa ya mikinda Mtwara Mjini Sababu ya kushambulia gari hilo ni
katika kile kinacho dhihirisha kua wana Mtwara bado hawajakubaliana na
hoja ya Serikali ya kutaka Kusafirisha Gesi hiyo kwaajili ya Manufaa ya
Nchi.
Lori hilo kwa sasa lipo kituo kikubwa cha polisi Mtwara, Ikiwa
ni
wiki moja tu imepita tokeaa watu kadhaa kukamatwa na jeshi la polisi
mkoani Mtwara kwa kile kinachodaiwa kusambaza waraka wa kuhujumu
miundombinuu yote ya gesi mara tu serikali itakapo anza utekelezaji wake
wa ujenzi wa bomba hilo kupeleka Dar.
WANANCHI WALISHAMBULIA KWA MAWE LORI LILILOBEBA MABOMBA YA KUSAFIRISHIA GESI HUKO MTWARA!
Friday, July 19, 2013
No comments
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment