TAHADHARI YA KIMBUNGA FELLENG KWA MTWARA NA LINDI.

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, TMA, inauhadharisha umma kuhusu hatari ya uwezekano wa kuwepo kwa mvua kubwa kwa baadhi ya maeneo nchini kutokana na kimbunga “FELLENG”.Baadhi ya maeneo ya mikoa ya Rukwa, Iringa, Mbeya, Njombe, Ruvuma, Morogoro, Pwani, Lindi, Mtwara na maeneo jirani ya mikoa hiyo huenda yakapatwa na mvua kubwa (zaidi ya milimita 50 katika kipindi cha saa 24 kila siku) kati ya tarehe 30 Januari, 2013 hadi 01 Februari, 2013.

0 comments:

Post a Comment