TAPELI ANAYETUMIA JINA LA WAZIRI LUKUVI AMTAPELI LOWASSA IRINGA

Tapeli  anayetapeli  watu maeneo mbali mbali ya Tanzania  kupitia jina la  waziri Lukuvi akiingizwa ktk  gari maalum leo
Tapeli  Jonathan Wiliam Lukuvi feki akitiwa matatani askari kanzu  Iringa
Mkuu  wa  mkoa  wa Iringa Dkt  Christina  Ishengoma ,askofu Dkt  Boaz Sollo na Waziri mkuu wa  zamani Edward  Lowassa akimsikiliza tapeli huyo akimpa maneno ya kitapeli  Lowassa
Kijana  huyo Tapeli akimsomesha  waziri Lowassa ukumbini kwa kuahidi kuchangia 100,000 huku akimwomba  kumsaidia misaada  zaidi
Hapa akipelekwa  katika gari maalum Hapa akiingizwa katika Taxi tayari  kwenda  polisi
Kijana ambae amekuwa akiwaliza  watumishi mbali mbali wa umma na watu  binafsi  kwa  kutumia jina la waziri wa nchi  ofisi ya  waziri mkuu  sera na uratibu  wa bunge kijana Jonathan Wiliam Lukuvi( si jina lake halisi)amekamatwa katika hafla ya kanisa la Overcomers FM akitaka  kumtapeli  waziri mkuu  wa zamani  Edward Lowassa kupitia harambee  hiyo.

"HAKUNA MWANAMKE KWENDA KWENYE SHOW YA DIAMOND HUKO LONDON"......MANGE KIMAMBI

Baada ya Diamond kusambaza clip ambayo inasikika Wema Akiongea nae ambayo Diamond Amesema kuwa Wema Alikuwa anajitongozesha...Mange Kimambi Ametoa Wito kwa wanawake wote walioko London Kutokwenda show ya Diamond akienda kufanya Show huko kwa vile alimzalilisha mwanamke mwanzao....


"Alafu bado utaona kunamijanamke huko London itavaa kabisa nguo na kujipaka ma makeup kwenye kumkatia Diamond viuno kwenye show... Ladies lets stand together...
tutadhalilishwa mpaka lini na hawa watu.....


Embu tuonyeshe mfano hapa......HAKUNA MWANAMKE KWENDA KWENYE SHOW YA DIAMOND HUKO LONDON..
                                                                                                  CHANZO MPEKUZI

WABUNGE WACHACHAMAA KUWA NYUMBA INAYOMILIKIWA NA MCHUNGAJI LWAKATARE IVUNJWE



'Hekalu' linalomilikiwa na Mchungaji Getrude Lwakatare.



Wabunge wamemtaka Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira Terezya Huvisa kuzivunja nyumba mbili zilizopo Mbezi Beach jijini Dar es Salaam zilizojengwa katika..


Bila kutaja majina ya wamiliki hao, wabunge hao walitaka hatua hizo zichukuliwe kwa haraka kwa nyumba hizo zilizojengwa kwenye fukwe kinyume cha sheria zivunjwe kwa maelezo kuwa hazina ofa wala hati. 
Sambamba na hilo wametaka watendaji wa serikali waliohusika kutoa vibali kuruhusu ujenzi huo kwa maelezo kuwa walichukua rushwa wachukuliwe hatua.
Mbunge wa kwanza kuanza kuzungumzia hilo ni wa viti maalum, Esther Bulaya (CCM) aliyetaja viwanja viwili vyenye namba 2019 na 2020 kikiwemo cha mbunge ambaye ni kiongozi wa kiimani waliojenga  nyumba zivunjwe licha ya kuwepo zuio la mahakama.
“Mwaka jana waziri wa Ardhi, Profesa Anna Tibaijuka alivunja nyumba za kawaida licha ya zuio la mahakama, lakini nyumba zilizo kwenye viwanja namba 2019 na 2020 hazikuvunjwa kwa sababu ya zuio la mahakama hii ni double standard hatuwezi kuvumilia.
“Wengine wenye nyumba ni viongozi tupo nao humu tena wa kiimani, lakini kwa nini viongozi tunafaya hivi wakati tunatakiwa tuwe wa mfano na tunawafanya viongozi wenzetu washindwe kufanya kazi zao?…hakuna haja ya kuogopa waziri Huvisa (Mazingira) vunja nyumba, haiwezekani kuwa na nguvu ya fedha.
“Wabunge wenzangu tuazimie Manispaa ya Kinondoni na NEMC (Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira), wakavunje nyumba hizo ndani ya wiki moja , naomba kutoa hoja,” alisema.
Hata hivyo, Spika Anne Makinda alimweleza; “Haiwezekani kutoa hoja kwa kuingilia vyombo vingine”.
Mbunge ambaye ni kiongozi wa kiimani mwenye nyumba katika  eneo hilo la Mbezi Beach aliyejenga katika fukwe ya bahari kwa kuondoa mikoko na kuweka kifusi na kujenga nyumba ni Mbunge wa Viti Maalumu, Mchungaji Dk. Getrude Lwakatare (CCM).
Naye Mbunge wa viti maalumu, Grace Kiwelu (Chadema) akichangia bajeti ya Ofisi ya Makamu wa Rais, alisema kamati yake ya Ardhi na Mazingira ilitembelea eneo hilo la Mbezi Beach na kukuta aliyejenga katika kiwanja 2019 hakuwa na ofa wala hati.
“Ametumia pesa kuwarubuni watendaji akaondoa mikoko, akaweka kifusi na akajenga nyumba naomba wizara ya Ardhi na ya mazingira wawachukulie hatua watendaiji hao,” alisema.

Akijibu hoja ya Bulaya, kuwa kwanini nyumba ya Mchungaji Lwakatare haikuvunjwa wakati nyingine zilivunjwa, mwanasheria mkuu wa Serikali, Frederick Werema alisema:

“Sisi ni wajibu wetu twende mahakamani kusema watu hao wamevunja sheria kujenga hapo. Wao wanaruhusiwa na Katiba na mahakama itafuata sheria.

“Nashauri Bulaya usitoe shilingi kuzuia Bajeti ya Waziri, uje tuone huyo kigogo itakuwaje.”
Hata hivyo, Huvisa alisema: “Nyumba tulizovunja hazikuwa na kesi na hii tuliyoiacha ilikuwa na kesi.”
Jumba la kifahari linalodaiwa kuwa la Mchungaji Lwakatare ambalo lilizinduliwa mwaka jana, limekuwa klikitajwa kuwa lina thamani ya takribani sh bilioni 1.5.
    zero99

LADY JAY DEE: "NAAMINI KABISA MUNGU SIO RUGE WALA KUSAGA. ATANISMIA KWENYE HILI #CONFIDENCE."

Baada ya mafumbo mengi na vijembe huko twitter na bbm hatimaye mwandana komandoo na super star Lady Jay Dee ameamua kufungua na kutaja majina ya hao watu wenye beef nae kupitia ukurasa wake wa twitter. Jide amefungua na kupodt yafuatyao. 

Dah naskia jana kwenya interview yake na TBC alimchana Ruge live, tunajaribu kuifuatilai interview hiyo na tutawaletea hapa live kila kitu alicho kiongela super star huyo. Stay tuned!


Kwa wale ambao hamuelewi mkasa huu pitia hii habari  hapa chini ambayo meneja wake Gardner Habash aliamua kufunguka na kuzungumzia tweet za mkewe huyo.


KUTOKANA na msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini Judith Wambura 'Lady JayDee' kuonekana kutuma 'Tweets' zilizobeba mafumbo huku akitoa mazito ya moyoni juu ya mtu anayemvurugia mipango yake ya kimuziki hakuweza kumtaja jina mume wake Gadna Habash afunguka juu ya 'Tweets' hizo



Akizungumza jijini Dar es Salaam hili hivi karibuni Gadna alisema kuwa 'tweets' alizoziweka msanii huyo zinalenga kufikisha ujumbe alioukusudia hususani kwa baadhi ya watu wanaomuwekea mipango mibaya ya kuharibu kazi zake za kimuziki



Alisema kuwa wapo baadhi ya washika dau wanaojikita katika maswala ya muziki kwa ajili ya maslahi yao binafsi huku wakimnyonya mwanamuziki bila ya kujali jasho lake na nguvu yake kwa kazi anayoifanya



Kutokana na hali ya kunyonywa wasanii na washika dau hao alisema msanii atakapopata akili na kuwa na uwezo wa kugundua kuwa ananyonya na hawezi kufika mbali hali inabadilika kwa kuanza kukandamizwa na kuwekewa vikwazo katika kazi zao



"Baadhi ya washika dau wanawaogopa wasanii wakubwa kwa kuwa tishio katika biashara zao hivyo hata wasanii wachanga pia wananyimwa nafasi ya kukua kisanii kwa kuhofia kuja kuwageuka baadaye pindi watakapopata nafasi ya kufanya hilo" alisema Gadna



Aliongezea kuwa mfumo wa muziki hauko sawa na upo kwa lengo la kumnyonya msanii hali ambayo inazidi kudidimiza wasanii na muziki wa nchi hii hali inayosababisha muziki unakuwa kwa kusikilizwa redioni na si kwa kukuwa kwa kipato kwa wasanii



Alisema kuna hujuma zinazoendelea kwenye soko la muziki zenye lengo la kumnyonya mwanamuziki na kumpa utajili mdau wa muziki sababu hiyo inapelekeea wanamuziki wa nchi yetu kutoendelea katika soko la muziki



Lady JayDee hivi karibuni amekuwa akitumia mtandao wa Twitter kwa ajili ya kutuma 'tweets' zenye ujumbe kwa mtu aliyemkusudia ingawa hazikuonyesha wazi wala kutaja jina la muhusaka



Hizi hapa chini ni baadhi ya 'tweets' zilizotumwa na msanii huyo hapo nyuma



Lady JayDee ?@JideJaydee

Hata nyimbo zisipopigwa now mi sio underground, won't complain. Nani asiemjua JayDEe? Am not crazy



Lady JayDee ?@JideJaydee

Basi mjue kuwa tatizo langu sio nyimbo kutopigwa redioni. Its more than that. U dig??



Lady JayDee ?@JideJaydee

Now nategemea nguvu ya uma #diehardfans



Lady JayDee ?@JideJaydee

Na tweet hivi sbb sikuwahi kulalamika nikaamua kufanya kazi. Lakini kazi inapowekewa uzito wa jiwe isipenye. That's another case...


MAREKANI IMEKUMBWA TENA NA MKASA MWINGINE, ARDHI IMEMEZA MAGARI KWA NAMNA HII

.
Hili tukio limetokea jana Alhamisi huko Chicago katikati ya makazi ya watu ambapo ni dereva mmoja tu ndio alijeruhiwa, chanzo ni kupasuka kwa bomba la maji hivyo ardhi ikajaa sana maji.

.

.
.

BAADA YA JUMA NATURE KUSHINDWA KUFANYA INTERVIEW JANA KATIKA TV KUTOKANA NA KUVAA NDALA NA AKIWA AMEKUNYWA POMBE ,HII NDIYO KAULI YAKE.


MSANII Nguli wa muziki wa Bongo Fleva Juma Kasim Kiroboto a.k. Sir nature,Kibla jana usiku alikuwa na Interview ya TV, lakini ilihailishwa baada ya msanii huyo kufika pale akiwa amevaa ndala na akiwa amekunywa pombe,

Ameumia sana kitendo cha kutofanya interview kwakuwa alivaa ndala na kaamua kusema hiviii "Kweli nilienda kwenye interview nimevaa ndala. Lakini niambie angeenda mzungu pale na ndalawangesitisha mahojiano? Sawa kunywa nilikuwa nimekunywa lakini kuna kibaya niliongea? Mbona mtangazaji alikuwa kavaa hovyo tu? Wamenikera na ngoma zangu sipeleki tena hata moja pale."
 Hivyo ndivyo Nature alivyosema Tomaoni yako shabiki wa Muziki na Shabiki wa Juma Nature