PROFESSOR JAY AFIWA NA MAMA YAKE MZAZI.


 

Kwa Mujibu Wa Gardner G Habash aliye kuwa karibu na rapper Profesa Jay, Leo Jioni Walipata taarifa kuwa mama yake mzazi amepata ajali na yupo kituo cha polisi akichukua PF3 ili akapate matibabu. Baada ya Profesa kupokea simu, palianza kuwa na tatizo la mawasiliano, Profesa alimpigia simu Mama yake mzazi na ndipo alipo mwambia Profesa kuwa ni kweli amepata ajali na anakwenda hospitalini. 

Katikati ya ule muda aliotumia Profesa Kufika Hospitalini, Mama Yake Mzazi Bi Rosemary Majanjara Alifariki Dunia. Pole kwa Familia Ya Profesa Jay, Ndugu na Marafiki Zao.

Pole sana Profesa Jay kwa kuondokewa na Mama yako kipenzi. Mungu akutie nguvu katika kipindi hiki kigumu

0 comments:

Post a Comment