Staa huyu wa Kenya apata pigo kubwa, Ampoteza baba yake mzazi


Habida Moloney, Staa wa muziki kutoka Kenya ambaye kwa sasa anatamba kwenye airwaven na ngoma/video yake ya 'Lights Up' yupo katika kipindi kigumu kwa wakati huu baada ya kumpoteza baba yake mzazi wiki hii katika Hospitali ya Aga Khan huko jijini Nairobi Kenya.
Msanii huyu ameamua kuweka maneno yafuatayo katika mtandao kushare hisia zake za upendo pamoja na huzuni kubwa ambayo imempata kwa kuondokewa na baba yake.
“To the greatest Husband, Father, Brother, Grandfather and much more. I love you and miss you dearly. May you rest in peace and may you be right there near the Lord. Good bye daddy”.
Mazishi ya mzee huyu yatafanyika siku ya Jumanne tarehe 30th July 2013 katika makaburi ya Lang’ata.

0 comments:

Post a Comment