WATU WAMSHAMBULIA DJ WA CLOUDS FM..DJ PQ BAADA YA KUTO PIGA nyimbo za Tanzania ndani ya BBA



DJ PQ ashindwa kupiga nyimbo za
Tanzania ndani ya BBA

jana usiku ilikuwa zamu ya DJ kutoka Tanzania
kuwaburudisha washiriki wa shindano la Big
Brother Africa. Kwa kawaida Multichoice huwa


wanaaalika maDJ kutoka nchi wa
shiriki kila jumamosi saa 5 mpaka saa 6 usiku
kuwarusha majoka washiriki wa BBA.jana usiku DJ kutoka Tanzania ambaye pia ni radio DJ
wa Clouds FM, DJ PQ alipata nafasi ya kuwa
burudisha washiriki. Cha ajabu huyu DJ
ameonesha kutokuwa mzalendo wa hali ya juu kabisa
kwa kutopiga nyimbo ya Tanzania hata moja
zaidi ya nyimbo ya mshiriki kutoka Tanzania
aitwaye Feza kama dedication kwake.
Badala yake 80% kapiga nyimbo za Nigeria
hasa za Psquare. Hili limenishangaza sana
kwani hakuna nyimbo yoyote ya bongo flava
yenye hadhi ya kupigwa ndani ya jumba la
BBA?
Mbona ma DJ wengine waliotangulia wiki za
nyuma walipiga nyimbo mbili ama tatu za
nchini mwao? Hata DJ wa Kenya alipiga za
kwao pamoja na Tanzania mfano alipiga
nyimbo ya Kesho ya Diamond na ya AY.
Tafsiri yangu ni kuwa huyu DJ hana
confidence kabisa, licha ya mabosi wake
Clouds FM kuhubiri umuhimu wa kutumia
vizuri fursa "opportunity" lakini huyu DJ somo
halijamuingia.
Hii inafanya watizamaji wa nchi zingine wahisi
kwamba Tanzania hakuna wanamuziki na
kwamba tuwasikiliza Psquare tu.
Ngoja nikope msemo wa Clouds FM kwa kumalizia "MADE IN TANZANIA".

0 comments:

Post a Comment